Luka 24:
(Luke)
13. Na tazama, siku ile ile watu wawili miongoni mwao walikuwa wakienda kijiji kimoja, jina lake Emau, kilichokuwa mbali na Yerusalemu kama mwendo wa saa mbili.
—————
Now behold, two of them were traveling that same day to a village called Emmaus, which was seven miles from Jerusalem.
14. Nao walikuwa wakizungumza wao kwa wao habari za mambo hayo yote yaliyotukia.
—————
And they talked together of all these things which had happened.
15. Ikawa katika kuzungumza na kuulizana kwao, Yesu mwenyewe alikaribia, akaandamana nao.
—————
So it was, while they conversed and reasoned, that Jesus Himself drew near and went with them.
16. Macho yao yakafumbwa wasimtambue.
—————
But their eyes were restrained, so that they did not know Him.
17. Akawaambia, Ni maneno gani haya mnayosemezana hivi mnapotembea? Wakasimama wamekunja nyuso zao.
—————
And He said to them, “What kind of conversation is this that you have with one another as you walk and are sad?”
18. Akajibu mmoja wao, jina lake Kleopa, akamwambia, Je! Wewe peke yako u mgeni katika Yerusalemu, hata huyajui yaliyotukia humo siku hizi?
—————
Then the one whose name was Cleopas answered and said to Him, “Are You the only stranger in Jerusalem, and have You not known the things which happened there in these days?”
19. Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, aliyekuwa mtu nabii, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote;
—————
And He said to them, “What things?” So they said to Him, “The things concerning Jesus of Nazareth, who was a Prophet mighty in deed and word before God and all the people,
20. tena jinsi wakuu wa makuhani na wakubwa wetu walivyomtia katika hukumu ya kufa, wakamsulibisha.
—————
and how the chief priests and our rulers delivered Him to be condemned to death, and crucified Him.
21. Nasi tulikuwa tukitumaini ya kuwa yeye ndiye atakayewakomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu yalipotendeka mambo hayo;
—————
But we were hoping that it was He who was going to redeem Israel. Indeed, besides all this, today is the third day since these things happened.
22. tena, wanawake kadha wa kadha wa kwetu walitushitusha, waliokwenda kaburini asubuhi na mapema,
—————
Yes, and certain women of our company, who arrived at the tomb early, astonished us.
23. wasiuone mwili wake; wakaja wakasema ya kwamba wametokewa na malaika waliosema kwamba yu hai.
—————
When they did not find His body, they came saying that they had also seen a vision of angels who said He was alive.
24. Na wengine waliokuwa pamoja nasi walikwenda kaburini wakaona vivyo hivyo kama wale wanawake walivyosema, ila yeye hawakumwona.
—————
And certain of those who were with us went to the tomb and found it just as the women had said; but Him they did not see.”
25. Akawaambia, Enyi msiofahamu, wenye mioyo mizito ya kuamini yote waliyoyasema manabii!
—————
Then He said to them, “O foolish ones, and slow of heart to believe in all that the prophets have spoken!
26. Je! Haikumpasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake?
—————
Ought not the Christ to have suffered these things and to enter into His glory?”


Leave a comment